Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani CCM wamfurusha mwenzao kikaoni
Habari za Siasa

Madiwani CCM wamfurusha mwenzao kikaoni

Spread the love

MADIWANI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, wamemtimua mwenzao kikaoni kwa kutovaa sare za chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga … (endelea).

Seleman Segreti, Diwani wa Nyida na wajumbe wengine watatu ndio waliokutwa na mkasa huo baada ya kuelezwa, kukiuka makubaliano ya kuvaa sare za chama hicho, kila wakati panapokuwa na kikao.

Emmanuel Lukanda, Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM wa Wilaya ya Shinyanga, ndiye aliyesimamia zoezi la kuwatimua wajumbe hao kabla ya kuanza kwa kikao.

Kabla ya kuanza kikao hicho, Lukanda alieleza kushangazwa na hatua ya wajumbe hao kuhudhuria kikao hicho bila kuvaa sare hizo kama walivyokubaliana.

“….hapa naona baadhi yenu hamjavaa sare,” alisema Lukanda na kuongeza “baadaye mtaandika barua za kujieleza kwanini hamkuvaa sare.” Hata hivyo, kikao hicho kiliahirishwa.

Utetezi alioutoa Diwani Segret, alisema hakulala nyumbini kwake kwa kuwa, alikuwa na mgonjwa Shinyanga Mjini, huko ndio alikolala na aliporudi alikwenda moja kwa moja kikaoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!