Madereva wa Daladala kituo cha Simu 2000, Manispaa ya Ubungo jijini Dar es salaam, wamekubali kumaliza mgomo waliouanza mapema leo asubuhi kutokana watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kutoa agizo la kupanda kwa bei ya Ushuru kutoka Sh 500 hadi Sh 1000, anaandika Irene David.
Mstahiki Meya Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob, ameagiza kurudi kiasi kilikile cha shilingi 500 kwa siku kwa kila daladala kwa kuwa baraza la madiwani halikuongeza kiasi hicho.
“Nimesikitishwa na watendaji wetu wa Halmashauri kutuingiza kwenye mgogoro na watumiaji wa huduma hii bila sababu za msingi, kwamba wana amka na kuongeza ushuru kutoka kiasi cha sh 500 mpaka sh 1000 bila kujua kuwa sheria hairuhusu jambo hilo.” Amesema Meya.
Meya amesema hatua kali za kinidhamu zitatolewa kwa waliopandisha kiasi hicho kwa kuwa baraza la madiwani halikuongeza kiasi hicho kama sheria ilivyo na baadae mabadiliko hayo kusainiwa na Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mkoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ndipo ianze kutumika.
Leave a comment