Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madaktari wapya; JPM atoa masharti
Habari za Siasa

Madaktari wapya; JPM atoa masharti

Spread the love

RAIS John Magufuli amemuagiza Kapteni Mstaafu , George Mkuchika,  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, kuajiri madaktari wapya 1,000. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 20 Februari 2020, wakati akihutubia katika maadhimisho ya siku ya madaktari Tanzania, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, ametoa masharti kwamba madaktari wanaotakiwa kuajiriwa, ni wale ambao waliokaa zaidi ya miaka mitano bila ajira. kwasasa, madaktari 2,700 hawana ajira nchini.

Kiongozi huyo wa nchi ameagiza madaktari hao watakapoajiriwa, wasambazwe nchi nzima hasa katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa mji.

“Nifahamu tuna madaktari 2,700 bado hawajaajiriwa nitaifanyia kazi, nafikiri tutaanza polepole hata tukaichukua 1000, tuanze na 1,000 mambo yakiwa mazuri tena tuendelea kuajiri. Sababu tuna hospitali vijijini wanahitaji madaktari, na hapa tunaajiri madaktari tu walioahangaika miaka 5. Na wasambazwe vizuri katika mikoa yote,” ameagiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo baada ya Dk. Elisha Osati, Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), kumuomba atatue changamoto ya ukosefu wa ajira kwa madaktari, pamoja na kuboresha masilahi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!