Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Madaktari Kenya kugoma tena
Kimataifa

Madaktari Kenya kugoma tena

Spread the love

MUUNGANO wa Wauguzi nchini Kenya umepanga kufanya mgomo kuanzia leo Jumatatu tarehe 4 Februari 2019 ili kuishinikiza serikali ya nchi hiyo kuwalipa stahiki zao ikiwemo marupu rupu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hii ni mara ya pili kwa muungano huo kuitisha mgomo, ikiwa mara ya kwanza madaktari na wauguzi nchini Kenya mnamo mwezi Novemba 2017 walifanya mgomo, lakini serikali ilifanya mazungumzo nao ndipo wakarejea tena kazini.

 Katibu Mkuu wa Muungano wa Wauguzi Kenya, Seth Panyako amesema serikali ya Kenya imeshindwa kutekeleza makubaliano yaliyoafikiwa mwezi Novemba 2017 katika kaunti nyingi ikiwemo kaunti ya Nairobi, Kisumu, Taita-Taveta, Kisii, Nyandarua, Elgeyo na Marakwet.

Amesema madaktari na wauguzi katika kaunti hizo hawataripoti kazini hadi pale makubaliano yao na serikali ya mwaka 2017 yatakapotekelezwa.

Kaunti ambazo madaktari na wauguzi wake hawatagoma kutokana na kulipwa stahiki zao ni pamoja na kaunti ya Mombasa, Migori na Machakos.

Hata hivyo serikali ya Kenya kupitia waziri wa Leba, Ukur Yatan amewataka wauguzi hao kusitisha mgomo huo kwa kuwa ameteua kamati itayakayoshughulikia masuala yao na kuandika ripoti ndani ya siku 30.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!