JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni asubuhi ya leo Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 walimkata Mgombea Ubunge wa Kawe, Halima Mdee wa Chadema kufuatia sintofahamu iliyojitokeza katika zeozi la upigaji kura jimboni humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa zinaeleza, Mdee alikamatwa katika Kituo cha Kawe kufuatia sintofahamu hiyo kutokea baada ya mgombea huyo kudai kuona masanduku ya kura yakiwa na kura zilizopigwa kinyume na utaratibu.
Akizungumzia sakata hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Edward Bukombe amesema, mgombea huyo alihojiwa baada ya kukamatwa kisha akaachiwa huru.
Kuhusu madai ya Mdee ya sanduku kukutwa na kura za kughushi, Kamanda Bukombe amesema hawajapokea taarifa hizo.
“Mdee yuko huru, kulikuwa na tafrani ikapelekea ahojiwe lakini baadae aliachiwa huru. Chanzo ilikuwa kutoelewana,” amesema
“Kwenye uchaguzi ni kawaida kuona mtu mabishano, kulitokea mabishano, ilikuwa ni kituo cha Kawe, bado taarifa za kuwa masanduku yalikuwa na kura bado hatujapokea,” amesema Kamanda Bukombe.
Leave a comment