Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Machozi ya Mbowe kwa JPM
Habari za SiasaTangulizi

Machozi ya Mbowe kwa JPM

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema. Picha ndogo Rais John Magufuli
Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, ametoa waraka maalumu kwa Watanzania kuonesha kilio chake kwa nchi ilipo na inapoelekea. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Waraka Maalum wa Freeman Aikaeli Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Hai kwa Taifa

Leo tarehe 22 Machi 2018, mimi na viongozi wenzangu waandamizi wa Chadema tumetakiwa tena kuripoti Polisi.

Tunaokabiliwa na usumbufu huu ni pamoja na: Mhe Vincent Mashinji (Katibu Mkuu), Mhe. John John Mnyika, Mb na Naibu Katibu Mkuu Bara, Mhe. Salum Mwalimu, Naibu Katibu Mkuu, Zanzibar; Mhe Halima J. Mdee, Mb, Mwenyekiti wa Bawacha, Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu, Mhe. John W. Heche, Mb, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Serengeti (Mara, Simiyu na Shinyanga) na Mjumbe wa Kamati Kuu; Mhe. Esther N. Matiko, Mb, Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Mara na Mweka hazina wa Bawacha Taifa.

Tuna taarifa pia ya kusudio la kumuunganisha Mhe. Peter Msigwa, Mb, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa (Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Iringa) na Mjumbe wa Kamati Kuu katika shauri hili.

Historia ya wito:

Kwa muda wa wiki tano sasa, kufuatia sintofahamu kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi wa marudio wa Jimbo la Kinondoni, Dar es Salaam na Siha, Kilimanjaro, tumekuwa tukisumbuliwa kuripoti Polisi kila wiki kwa mashtaka ambayo hayajawahi kuwekwa bayana.

Katika kampeni na chaguzi hizi, palijitokeza mambo mengi ya ukiukwaji wa Haki za binadamu, ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, matumizi mabaya ya madaraka ya kiserikali, udhalilishaji na unyanyapaa dhidi ya Vyama vya Upinzani, mauaji na mateso kwa viongozi wa vyama vya Upinzani na hata Wananchi wasio na hatia.

Wakati nenda rudi hii ikiendelea, tuna taarifa (asante teknolojia) kuwa zinapangwa njama mahususi za kutubambikia viongozi wa Chadema kesi za Mauaji au Uhaini ili kuhalalisha azma ya Watawala kutuweka mahabusu kwa muda mrefu, wakidhani kwa kufanya hivyo watakuwa wamefanikisha ku sha na hata kuua kabisa uwepo wa Upinzani katika Taifa.

Jitihada hizo ni pamoja na kujaribu kuhusisha viongozi, wanachama na wapenzi wa chama chetu na tuhuma aidha za Kigaidi, Mauaji na hata Uhujumu wa Uchumi.

Mkakati huukKitaifa unashinikizwa na Rais John Pombe Magufuli na kuratibiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, Dk Modestus Kipilimba, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, Jeshi la Polisi, na O si ya DPP.

“Viongozi” hawa, wasaidizi na washirika wao wamejazana matumaini hewa kuwa vuguvugu la mabadiliko na uhitaji wa demokrasia ya kweli na vita dhidi ya udikteta katika taifa hili litazimwa kwa “kuwa cha, kuwapoteza na hata kuwaua” viongozi wa Chadema na wanaharakati wengine wanaoamini katika uhalisia huu.

Naam, njama hizi zaweza kuua baadhi, kujeruhi baadhi na hata kupoteza kadhaa! Lakini kamwe, hazitazima njozi za Watanzania wema kupigania haki na ustawi katika nchi yao.

Naamini kwa kuzima uongozi wa Chadema uliopo leo, siyo tu kutaruhusu kuchipua kwa kasi kwa uongozi mbadala, bali pia kutaamsha ari ya taifa kuongeza juhudi katika harakati ili hatimaye kutokomeza udikteta na uongozi wa kiimla katika nchi yetu.

Taifa lina msiba! Wanasiasa, wanaharakati, wanahabari na hata wasanii wanateswa, wanafungwa, wanajeruhiwa na wengine kuuwawa! Wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani na nje wanalia! Viongozi wa dini wanachanganyikiwa! Wakulima, wafugaji na wavuvi wako hoi! Hata watoto na wanafunzi nao ni tishio kwa watawala!

Taifa limejazwa hofu. Wengi hawasemi, lakini wanataabika rohoni. Wanaisubiri fursa iwavyo vyovyote vile.

Nguvu, majeshi na silaha zao, magereza na mifumo kandamizi haziwezi kuwa suluhu ya uimla huu. Tuimarishwe badala ya ku shwa.

Hatukimbii!! Tuko tayari kwa lolote, popote!

Shime Watanzania! Msitulilie! Lilieni watoto wenu na Taifa la kesho.

Na iwe vyovyote iwavyo! Damu, mateso, dhihaka dhidi ya maisha yetu iwe chachu ya dhati katika kutafuta Tanzania aliyoikusudia Mwenyezi Mungu yenye kusimamia haki, demokrasia, usawa, utu na ustawi kwa wote!!

Aluta Continua!!!

Freeman Aikaeli Mbowe

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!