Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Machafuko yakosesha watoto elimu DRC 
Kimataifa

Machafuko yakosesha watoto elimu DRC 

Watoto nchini Kongo
Spread the love

ASASI isiyo ya kiserikali nchini kongo imesema  watoto wengi zaidi wanakosa elimu kutokana na mgogoro na mfumo duni wa elimu wa nchi hiyo. anaandika Victoria chance.

Ripoti ya Baraza la Wakimbizi la Norway imebainisha kuwa  asilimia 92 ya watoto wenye umri wa miaka sita hadi 11 wamekosa elimu katika miji iliyokumbwa na machafuko ya Kalemie na Tanganyika.

Shule 900 zimebomolewa kutokana na kushamiri kwa machafuko katika mkoa wa Kasai katikati mwa Kongo DRC katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Asasi hiyo imetahadharisha pia kwamba nchi hiyo kubwa ya katikati mwa Afrika inakabiliwa na hatari ya kupoteza kizazi chake kijacho kwa sababu katika mwaka huu umetolewa mchango wa asilimia nne tu ya fedha za misaada ya kibinadamu kwa ajili ya sekta ya elimu ya Kongo DRC.

Baraza la Wakimbizi la Naorway limeongeza kuwa watoto waliotimiza umri wa kwenda shule wanachangia zaidi ya asilimia 17 ya watu wapatao milioni 3.8 waliopoteza makaazi yao nchini humo katika  kipindi cha miongo miwili iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!