Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mabula aonesha njia utatuzi mgogoro wa ardhi Mara
Habari Mchanganyiko

Mabula aonesha njia utatuzi mgogoro wa ardhi Mara

Angeline Mabula, Mbunge wa Ilemela, Mwanza
Spread the love

NAIBU Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula ameagiza zoezi la kupima upya mipaka ya vijiji vya Kono na Ketembere kuanza haraka. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Vijiji hivyo vipo katika Kata ya Nata na Rigicha wilayani Serengeti Mkoa wa Mara ambapo ameagiza ifikapo Desemba 2018, ramani ya mipaka ya vijiji hivyo iwe imekamilika na kutolewa.

Agizo la Mabula linafuatia mgogoro wa muda mrefu uliokuwepo baina ya mipaka ya vijiji hivyo jambo linalosababisha shughuli za maendeleo ikiwemo mpango wa matumizi bora ya ardhi kushindwa kufanyika.

Akiwa katika ziara yake ya kutatua mgogoro huo,Mabula amesema, mgogoro wa mpaka baina ya vijiji hivyo ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi kushindwa kufuata taratibu za kupima mipaka kwa kuwashirikisha wananchi wa pande zote mbili.

“Makosa yaliyofanywa na ofisi hayawezi kuleta ugomvi katika vijiji hivyo na ramani ya eneo hili itarekebishwa kulingana na dira na wizara itaangalia namna ya kushughulika na waliokwepesha mipaka ili kujua walikuwa na maana gani” amesema Mabula.

Kwa mujibu wa Mabula lengo la kupima mipaka ni kuwezesha kuwepo mpango wa matumizi bora ya ardhi ambapo kupitia mpango huo wananchi wataweza kupatiwa hati miliki ikiwemo hati za kimila kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi na kusisitiza kuwa ardhi ndiyo mtaji pekee kwa wananchi wa vijiji hivyo.

Awali aliwapa nafasi  wananchi wa vijiji vya pande zote mbili kueleza jinsi wanavyoifahamu mipaka ya vijiji vya Kono na Ketembere ambapo wengi waliutambua Mto Masara kama mpaka wa vijiji hivyo.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kono, Michael Oyatason amesema, vijiji hivyo awali havikuwa na mgogoro wowote ila tatizo lilianza mara baada ya uwekaji alama za mipaka ambao haukushirikisha pande zote mbili kinyume kabisa na utaratibu wa kuainisha mipaka.

Mpima Ardhi Kanda ya Simiyu, Godwin Saiguran amemuahidi  Mabula kuwa zoezi la uanishaji mipaka ya vijiji vya Kono na Ketembere  kwa kushirikisha wananchi wa pande zote mbili litakamilika ndani ya siku nne.

Katika hatua nyingine Mabula ametatua mgogoro mkubwa baina ya vijiji vya Kazi na Rwamchanga vilivyopo katika Kata ya Manchira, Wilaya ya Serengeti mkoani Mara.

Mgogoro katika eneo hilo unachangiwa na msuguani wa wananchi wanaotaka kuwa na vijiji viwili kama ilivyoainishwa katika mipaka ya kiutawala ama kuwa na kijiji kimoja.

Awali kabla ya kuzungumza na wananchi wa vijiji hivyo Mabula alizungumza na wajumbe wa serikali ya vijiji ambapo alipowahoji viongozi wanaotaka kuwepo kijiji kimoja ama viwili ni wajumbe wawili kati ya nane waliokuwa wakihitaji kijiji kimoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

error: Content is protected !!