JUMLA ya Mabalozi 63 wameshakabidhiwa maeneo ya kujenga ofisi zao Katika Jiji la Dodoma lakini Ubalozi wa Zambia tayari umeshaanza mchakato huo kwa kuanza ujenzi wa nyumba ya Mkandarasi wake. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi wakati akitambulisha mpango wa maonyesho ya wajenzi katika mkakati wa ‘Tunajenga Dodoma.’
Kunambi amesema mabalozi hao walikwenda wiki mbili zilizopita lakini juzi balozi wa Zambia akamuomba kumpatia kiwanja cha kununua haraka kwa ajili ya kujenga nyumba ya mkandarasi atakayekuwa akisimamia jengo la ubalozi.
Amesema mkakati umewekwa kwa ajili ya kuijenga Dodoma mpya itakayolingana na miji ya Abuja (Nigeia), Pretoria (Afrika ya Kusini) au Mji wa Nairobi nchini Kenya na kwamba Serikali imekwishatoa kiasi cha Sh 1.2 bilioni kwa ajili ya mapitio ya ramani ambayo hata hivyo hayataruhusu nyumba za watu kubomolewa isipokuwa kama kuna umuhimu zaidi.
Akizungumzia kuhusu vifaa vya ujenzi kwamba havitoshelezi, Meneja wa Tawi wa mabati ya Alaf Grayson Mwakasege, amesema dhata kuwa vifaa vya ujenzi kwa Dodoma ni vichache si ya kweli na kuwa imepitwa na wakati kwani bidhaa ipo ya kutosha isipokuwa watu wanatumia mwanya huo kutaka kuhalalisha manunuzi nje ya mkoa.
Mwakasege amesema ujenzi wa jiji hilo jipya hauwezi kumaliza malighafi iliyopo ambayo kila soko linavyopanuka ndivyo ambavyo wafanyabiashara wanavyoendelea kuongeza mitaji yao na kupeleka bidhaa hitajika.
Leave a comment