Wizara ya Nishati na Madini imefanya mabadiliko kufuatia kupitishwa kwa sheria mpya ‘the written laws (miscellaneous amendmend ) Act 2017 iliyofanyiwa marekebisho kadhaa katika sheria ya mwaka 2010, anaandika Victoria Chance.
Marekebisho hayo ni kuanzishwa kwa tume ya madini, kufutwa kwa wakala wa ukaguzi wa madini, kuongezeka kwa malipo ya mrabaha asilimia nne(4%) hadi asiliia sita(6%), kwa madini ya metali na kuongeza kwa kwa malipo ya mrabaha kutoka asilimia tano(5%) hadi sita(6%) kwa almasi na vito.
Pia kupitia marekebisho ya sheria ya fedha na kodi, kila kampuni au mtu atakayesafirisha madini nje atalipia ada ya ukaguzi ambayo ni asilimia moja ya thamani ya madini yake na hata wachimbaji wadogo watalipia asilimia tano (5%) ya thamani ya madini yake ikiwa kama kodi ya zuio.
Aidha, katika suala la kufutwa kwa TMAA na ofisi za madini za kanda wizara imesema watumishi wataendele kufanya kazi kwani hawana tuhuma zozote na katika kipindi ambapo tume ya madini haijaundwa shughuli za tume zitafanywa chini ya kamishna wa madini .
Hata hivyo, wizara imewasisitiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano hasa katika kipindi hiki cha mpito wakati serikali imesimamisha utoaji wa leseni za utafutaji na uchimbaji wa madini hadi hapo tume ya madini itakapoundwa.
Leave a comment