Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Maambukizi ya VVU yapiga kambi kwa wanandoa
Habari Mchanganyiko

Maambukizi ya VVU yapiga kambi kwa wanandoa

Spread the love

WATU waliofunga ndoa na kuunganika kuwa kama mwili mmoja na kuepukana na masuala ya kufanya ngono zembe, imebainishwa wao kwa sasa ndio wamekuwa vinara wa kupata maambukizi mapya ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), kutokana na kutozingatia sheria na kanuni za ndoa, ananadika Mwandishi Wetu.

Imeelezwa kuwa watu wamekuwa wakiingia kwenye ndoa kama fasheni, bila ya kufahamu nini maana ya kufunga pingu hizo za maisha, na kujikuta baada ya muda mfupi wamechokana na kuanza kufarakana.

Hayo yalizungumzwa juzi na mwandishi wa kitabu cha Sakramenti ya ndoa katika nyumba aminifu Paschal Maziku, wakati akikitambulisha kwa waumini wa Kanisa Katoliki mjini Shinyanga.

“Tulifanya utafiti na kugundua wanandoa ndio wamekuwa vinara wa maambukizi mapya ya VVU, ambapo kisheria wanandoa ndio wanapaswa kuwa salama sababu kabla ya kufunga pingu za maisha huwa wanapimwa afya zao, lakini kwa hali ya sasa imebadilika na wengi wao ndio
waathirika wa Ukimwi,” amesema Maziku

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!