MAALIM Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo amesema, chama hicho kimejiandaa kushika dola na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kijiandae kuondoka ‘taka isitake’ baada ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Faki Sosi, Lindi … (endelea)
Maalim Seif ametoa kauli hiyo leo Jumanne tarehe 1 Septemba 2020 katika mkutano wa uzinduzi wa kampini za urais katika Uwanja wa Shule ya Msingi Mpilipili.
Bernard Kamilius Membe ndiye mgombea urais na Profesa Omar Fakih Hamad, mgombea mwenza.
Akizindua kampeni hizo, Maalim Seif amesema, msimamo wa chama hicho sasa ni kukataa kuonewa.
Amesema wagombea wa ACT-Wazalendo wa Tanzania Bara na Zanzibar.
“Chama cha ACT-Wazalendo sasa kimekuwa ni tishio kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndio maana wagombea wetu wameenguliwa, msimamo wetu sasa maonevu basi,” amesema Maalim Seif ambaye ni mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama hicho.
“Sasa huu ni wakati wa kuikomboa nchi yetu na mkombozi ni ACT-Wazalendo, tunahitaji serikali itakayoleta maendeleo kwa wananchi, itakayoleta uhuru kwa wananchi na Serikali hiyo itaongozwa na Bernard Kamilius Membe,” amesema Maalim Seif huku akishangiliwa.
Leave a comment