Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif awakaribisha wanaotaka kumweka pingamizi
Habari za Siasa

Maalim Seif awakaribisha wanaotaka kumweka pingamizi

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mgombea Urais Zanzibar kupitia ACT- Wazalendo amewakaribisha wale wote ambao wanataka kumwekea pingamizi Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufanya hivyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Unguja … (endelea).

Maalim Seif ametoa kauli hiyo jana Jumanne tarehe 8 Septemba 2020 alipozungumza katika Kongamano la Vijana wa ACT-Wazalendo visiwani humo.

Tayari Maalim Seif amekwisha kuchukua fomu za utezi wa kugombea urais ZEC katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020.

Fomu hizo amezirejesha leo Jumatano tarehe 9 Septemba 2020.

Amesema, kuna watu wa vyama vingine wamepanga kumwekea mapingamizi ZEC ili asiteuliwe kugombea.

Maalim Seif ambaye pia ni Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo anawakaribisha watu wanaotaka kumwekea pingamizi akisema anafahamu namna ya kupangua mapingamizi yao.

“Nasikia kuna watu washapangwa na vyama vingine kuniwekea pingamizi, nawakaribisha sababu kuniwekea pingamizi yeye anakuja kutoa haja zake na ushahidi wake na mimi naujua vilevile.”

“Sioni kama kuna pingamizi yoyote, kama itasimama juu yangu. Mimi nimezaliwa Mtambwe hamjui ninyi? Ndiyo sifa ya kwanza ya mgombea urais awe Mzanzibar wa kuzaliwa sio Mzanzibar mkaribishi,” amesema Maalim Seif.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!