Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif apigwa ‘stop’ Clouds TV
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif apigwa ‘stop’ Clouds TV

Spread the love

MAMLAKA katika kituo cha televisheni cha Clouds, jijini Dar es Salaam, imeagiza kufutwa kwa mahojiano kati ya kituo hicho na mwanasiasa mkongwe Visiwani Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mahojiano kati ya Maalim Seif na kituo hicho, yalipangwa kufanyika leo, tarehe 28 Machi na kurushwa moja kwa moja (live), kupitia kipindi kilichopewa jina la Clouds 360.

Kwa mujibu wa Ado Shaibu, katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama cha ACT-Wazalendo, televisheni ya Clouds ndiyo iliyoomba kuwapo mahojiano hayo na Maalim Seif.

Anasema, “Clouds TV imefuta ratiba ya mahojiano hayo kwa kile walichoeleza, sababu zilizo nje ya uwezo wao.”

Maalim Seif ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) na Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Alijiunga na ACT- Wazalendo na kukabidhiwa kadi ya heshima ya mwanachama Na. 1, mapema wiki iliyopita, kufuatia Mahakama Kuu, kumtangaza Prof. Ibrahim Lipumba, kuwa mwenyekiti halali wa chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!