Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif amfuata JPM Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif amfuata JPM Ikulu

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, ametinga Ikulu, jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Muda mfupi baada ya kukutana na Rais Magufuli leo tarehe 3 Machi 2020, Maalim Seif ameeleza kuwa wamezungumzia masuala ya nchi na namna ya kufanya amani iendelee kuwepo.

“Tumekutana na kubwa tumezungumzia mambo ya nchi yetu, vipi tutaendelea kuifanya Tanzania iwe na amani, nchi ya salama na upendo kwa Watanzania wote,” amesema Maalim Seif na kuongeza:

“Ni mtu muwazi na anapenda kukutana na watu, nafurahi sana kwa rais anakubali kukutana na raia wake…, namshukuru rais kakubali tukutane, tuzungumze mambo ya maslahi ya nchi yetu.”

Hata hivyo, Maalim Seif ameeleza kwamba, mengine aliyoongea na rais yatabai ndani na hayawezi kupelekwa kwa jamii “mengine tumezungumza humo ndani mimi na rais, huwezi kuyasema public (wazi), bila shaka kukiwa na haja ya kukutana, tutakutana tena.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!