Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif akamatwa Z’bar 
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif akamatwa Z’bar 

Maalim Seif Sharrif Hamad, aliyekuwa Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Taifa
Spread the love

MGOMBEA Urais wa Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad inadaiwa amekamatwa na Jeshi la Polisi katika Kituo cha kupigia kura cha Garagara visiwani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Maalim Seif amekutwa na kadhia hiyo leo Jumanne tarehe 27 Oktoba 2020 ikiwa ni siku ya kwanza ya upigaji kura katika Uchaguzi Mkuu visiwani huo utakaohitimishwa kesho Jumatano.

“Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo Zanzibar, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa ACT-Wazalendo, Maali Seif Sharif Hamad amekamatwa muda huu na vyombo vya dola wakati akiwa katika kituo cha kupigia kura cha Garagara. Taarifa zaidi zitawajia,” inaeleza taarifa ya ACT-Wazalendo.

Taarifa ya chama hicho inasema, Maalim Seif amepelekwa Kituo cha Polisi Ziwani kwa mahojiano.

Maalim Seif Sharrif Hamad, Mgombea Urais Zanzibar kwa tiketi ya ACT-Wazalendo

Sheria ya uchaguzi ya Zanzibar inaruhusu watumishi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na watumishi wengine watakaosimamia Uchaguzi Mkuu wa kesho Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 kupiga kura siku moja kabla ya uchaguzi.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari mbalimbali ikiwemo kauli ya Jeshi la Polisi kuhusu suala hili.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!