Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif aichamba CCM
Habari za Siasa

Maalim Seif aichamba CCM

Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa CUF. Picha ndogo Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) amesema kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM) sio chama cha kukimbilia.  Anaripoti Regina Kelvin …(endelea).

Amesema, haoni sababu mtu mwenye msimamo imara kukimbilia kwenye chama hicho na kwamba, mfumo wa uendeshaji wake haukidhi wara kuridhisha.

“Siridhishwi hata kidogo na utendaji wa CCM” amesema Maalim Seif alipokuwa Kilimahewa visiwani Zanzibar wakati akizindua Jumuiya ya Wazee wa chama hicho (JUZECUF) jana.

Amesema kuwa, hana ndoto ya kujiunga na CCM ambayo utendaji wala mwelekeo wake kwa taifa hauelewiki.

Maalim Seif ameeleza kuwa, kinachotokea katika serikali inayoindwa na CCM hasa kukamatakamata hovyo hakijawahi kutokea hata wakati wa Ukoloni.

“CCM inatakiwa kuelewa haiwezi kutawala nje ya mfumo ambao Watanzania wanavyotaka nchi yao itawaliwe,” amesema na kuongeza;

“Mara kwa mara unasikia diwani ama mbunge kaingia CCM, tena kwa kutoa tamko maalumu. Haya mliyaona wapi?” amehoji Malim Seif.

“Imefika hatua sasa Mwenyekiti wa Kijiji kwa kuwa tu anatoka CCM basi anaweza kuamrisha Jeshi la Polisi likukamate na unakamatwa kweli na kuwekwa ndani,”amesema Maalim Seif.

Katika mazungumzo na wazee hao Maalim Seif amegawa kadi kwa wanchama wapya huku akiahidi kuendelea kuimarisha chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!