UHURU wa kiuchumi kwa Wazanzibari kupitia zao la Karafuu, sasa utapatiwa ufumbuzi kwa wakulima kuuza kokote watakapo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zamzibar … (endelea).
Ni kauli ya Maalim Seif Sharif Hamad, mgombea urais visiwani Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo aliyoitoa kwenye mkutano wake wa kampeni katika Kijiji cha Konde, Pemba.
“Tunataka wakulima wetu watangaze, waitangaze Zanzibar katika soko la ulimwengu na wafanyabiashara ya viungo watoke huko waje Zanzibar.”
“Tutawapa mbinu wakulima wetu ili wazalise bidhaa zilizo bora zaidi. Tutakusanya kodi kidogo ili wakulima watate faida kubwa na pia kuendeleza kilimo kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu,” amesema Maalim Seif.
Akielezea hali ya wakulima hao, Maalim Seif ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho amesema, wakulima hao wanaandamwana na kodi kubwa ya mazao yao huku serikali ikishindwa kuwaandalia mazingira mazuri ili wafanye kilimo chenye tija.
Leave a comment