Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif agombea uenyekiti ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Maalim Seif agombea uenyekiti ACT-Wazalendo

Hayati Maalim Seif Sharif Hamad
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, mshauri mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho. Anaripoti Jabir Idrisa, Zanzibar…(endelea).

Kiongozi huyo nguli wa siasa za upinzani Zanzibar, amechukua fomu hiyo leo tarehe 30 Januari 2020, katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Vuga, Unguja.

Doroth Semu, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho ndiye aliyemkaribisha na kumkabidhi fomu Maalim Seif, huku akisema ‘nafasi zipo wazi kwa kila mwanachama aliyetimiza vigezo.’

Chama hicho, tarehe 27 Januari 2020, kilifungua mlango kwa wanachama wake walio na sifa, kujitokeza na kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.

Mbele ya vyombo vya habari, Maalim Seif amesema, amejitokeza kuchukua fomu hiyo kwa kuwa, ana haki ya kufanya hivyo kama ilivyo kwa wanachama wengine wa chama hicho.

Na kwamba, anao uwezo na uzoefu wa muda mrefu katika masuala ya siasa na uongozi, hivyo anaamini nafasi hiyo ni muafaka kwake hasa katika kipindi hiki.

Amesema, kujitokeza kwake kuchukua fomu hiyo kunatokana na malengo yake ya kufanyia mabadiliko makubwa ya chama hicho, “kama wanachama wataniridhia kuwa mwenyekiti, nitasimamia uwajibikaji na nidhamu ndani ya chama.”

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!