Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maadhimisho Uhuru yaahirishwa, JPM atoa maagizo
Habari za Siasa

Maadhimisho Uhuru yaahirishwa, JPM atoa maagizo

Jengo la Hospitali ya Uhuru inayojengwa na Serikali katika wilaya Chamwino, Dodoma
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli ameahirisha maadhimisho ya 59 ya sherehe za Uhuru wa Tanzania Bara zilizokuwa zifanyika tarehe 9 Desemba 2020. Anaripoti Brightness Boaz, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli ameelekeza fedha Sh.835.4 milioni zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe hizo zitumike kununulia vifaa mbalimbali kwenye Hospitali ya Uhuru jijini Dodoma.

Taarifa iliyotolewa na ofisi ya waziri mkuu leo Alhamisi tarehe 3 Desemba 2020 imesema, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa taarifa hiyo kwenye sherehe za kuadhimisha miaka 60 ya kuanzishwa kwa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) zilizofanyika jijini Dar es Salaam.

Majaliwa amesema, Rais Magufuli ameagiza siku hiyo itumike kwa ajili ya kufanya shughuli mbalimbali za kijamii nchini.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akikagua jengo la Hospitali ya Uhuru inayojengwa na Serikali katika wilaya Chamwino, Dodoma

Tarehe 20 Novemba 2018, Rais Magufuli aliagiza kiasi cha Sh.995.18 milioni zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya maadhimisho ya 57 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, zitumike kujenga Hospitali ya Uhuru, ambayo kwa sasa ujenzi wake umefikia asilimia 92.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya 59 ya Uhuru wa Tanzania Bara kwa mwaka 2020 inasema; ‘Miaka 59 ya Uhuru na Miaka 58 ya Jamhuri: Tanzania yenye Uchumi Imara Itajengwa na Watanzania Wenyewe, Tufanye Kazi kwa Bidii, Uwajibikaji na Uadilifu.’

Waziri Mkuu amesema, hadi kufikia sasa ujenzi wa hospitali hiyo ya Uhuru umegharimu Sh.4.2 bilioni.

Januari 2019 wakati akipokea gawio la hisa za kampuni ya Simu ya Airtel, Rais Magufuli aliagiza kiasi cha Sh.2.41 bilioni zilizotolewa na kampuni hiyo zitumike katika ujenzi wa hospitali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!