Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Lulu ahukumiwa jela miaka miwili, ajipanga kukata rufaa
MichezoTangulizi

Lulu ahukumiwa jela miaka miwili, ajipanga kukata rufaa

Elizabeth Michael 'Lulu' akipanda gari kupelekwa gerezani muda mfupi kabla ya kusomewa hukumu yake
Spread the love

LEO, tarehe 13 Novemba 2017, mahakama kuu jijini Dar es Salaam, imemuhukumu kifungo cha miaka miwili gerezani, msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Micheal (Lulu). Anaripoti Faki Sosi ….(endelea).

Lulu amehukumiwa kifungo hicho baada ya kukutwa na hatia ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa mpenzi wake, Steven Kanumba.

Akisoma hukumu hiyo mbele ya mahakama iliyosheheni mamia ya wananchi, Jaji Sam Rumanyika alisema, “ushahidi wa upande wa mashtaka umejikita kwenye ushahidi wa kimazingira kwa kuwa Lulu ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kuwa na Kanumba.”

Alisema, ushahidi wa aina hiyo, unakuwa sio wa moja kwa moja, licha ya kuwa una vipande mithili ya nyololo ambavyo vimeshikana.

Akitoa maelekezo kwa wazee wa baraza waliokuwa wanasaidia mahakama kutenda haki, Jaji Rumanyika alisema, “…katika utoaji wa maoni yenu, sio lazima mthibitishe makossa. Lakini kama mkiona pia mshtakiwa hausiki basi msisite kuieleza mahakama.”

Kanumba aliuawa usiku wa tarehe 7 Aprili 2012, maeneo ya Sinza, Vatican, manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam.

Kabla ya kufikishwa mahakama kuu, Lulu alifikishwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, tarehe 12 Aprili 2017, ambako alisomewa shitaka hilo.

Jaji Rumanyika amesema katika uamuzi wake, amemtia hatiani Lulu, kwa kuzingatia kifungu cha 195 cha sheria ya makosa ya jinai.

 

 

Upande wa Jamhuri ulileta mahakamani mashahidi wanne wakiwemo Seth Bosco, mdogo wa Kanumba. Bosco alikuwa akiishi nyumba moja na marehemu na alikuwapo siku ya tukio.

Mwingine, ni Dk. Paplas Kagaiga, aliyekuwa daktari wa familia hiyo aliyefika nyumbani kwa marehemu Kanumba mara baada ya kudondoka.

Wengine, ni daktari kutoka kwenye hospitali ya taifa Muhimbili aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Kanumba pamoja askari ASP Ester aliyefanya upelelezi kwenye tukio hilo pamoja na kumtia mbaroni Lulu.

Lulu alikuwa anatetewa na wakili maarufu Peter Kibatala. Aliwasilisha mahakamani mashahidi wa wawili – Lulu mwenyewe na Josephine Mushumbuzi, mke wa aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema.

Lulu alieleza mahakama, akiwa chini ya kiapo, mazingira yote ya tukio hiilo kuapa kutohusika na mauaji dhidi ya Kanumba.

Mama mzazi wa Lulu akitoka mahakamani baada ya mtoto wake kusomewa hukumu

Naye Josephine ambaye ushahidi wake uliwasilishwa mahakamani kwa njia ya maandishi, alidai kuwa Kanumba alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo.

Akitoa maoni yake, mmoa wa wazee hao wa baraza, Omary Panzi alisema Lulu ameua bila kukusudia.

Kwamba maoni yake hayo yanatokana na ushahidi wa Bosco – mdogo wa Kanumba – aliyeleza jinsi ugomvi ulivyotokea baina ya wawili hao.

“Maoni yangu ni kwamba marehemu alikufa kwa sababu ya kuteleza ikizingatiwa ilikuwa ni usiku na kulikuwa na giza, na chanzo cha kutekeleza ni ugomvi wake na Lulu,” alieleza.

Mama mzazi wa Marehemu Steven Kanumba, akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutoka mahakamani

Naye Bi. Sarah  alisema Kanumba alikufa kutokana na ugomvi ambapo ushahidi pia umetueleza kulikuwa na giza.

“Hivyo Lulu hakuuwa makusudi. Ameuwa bila kukusudia,” alieleza.

Kwa upande wake, Rajabu Mlawa amesema, kutokana na yaliyoelezwa mahakamani, anaridhika bila chembe ya shaka kuwa Lulu ana kosa la kuuwa bila kukusudia.

Alisema, “ameuwa bila kukusudia na nimeridhika na kilichosemwa. Kanumba alikuwa na mwili mkubwa na alikuwa katika hali ya kulewa, hivyo inaonekana katika heka heka za ugomvi inawezekana Lulu alitumia nguvu kidogo ya kumsukuma hadi kudondoka.”

Wakili wa Lulu, Kibatala amesema wanajipanga kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Habari za SiasaTangulizi

CDF Mabeyo: Magufuli alijua anakufa

Spread the love  ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi nchini (CDF), Jenerali Venance Mabeyo,...

AfyaTangulizi

Serikali yafafanua kuondolewa dawa 178 kitita cha NHIF

Spread the loveSERIKALI imesema imeondoa dawa 178 katika kitita cha Mfuko wa...

error: Content is protected !!