Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lukuvi sasa kutembea mkoa kwa mkoa
Habari za Siasa

Lukuvi sasa kutembea mkoa kwa mkoa

Spread the love

WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameamua kutembea mkoa kwa mkoa ili kukabili migogoro ya ardhi nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Leo Alhamisi tarehe 22 Novemba 2018 atafanya ziara ya kushughulikia migogoro ya ardhi katika shamba la Singu na Endasagu yaliyopo Wilaya ya Babati, Mkoa wa Manyara ili kutatua migogoro katika mashamba hayo baina ya wamiliki na wananchi.

Uamuzi wa Lukuvi kufanya ziara katika mashamba hayo ni moja ya jitihada zake za kushughulikia migogoro ya ardhi kutokana na uwepo kero na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuhusiana na huduma za ardhi.

Akiwa wilayani Babati, Lukuvi atakagua mashamba ya Singu na Endasagu sambamba na kusikiliza malalamiko ya wananchi kuhusiana na mashamba hayo na baadaye kutafuta ufumbuzi.

Aidha, katika mfululizo wa kushughulikia migogoro ya ardhi, Lukuvi mara baada ya kurejea kutoka mkoani Manyara atafanya ziara katika halmashauri zote za mkoa Dar es Salaam,Wilaya za Kinondoni, Ilala, Kigamboni, Ubungo na Temeke ambapo mbali na mambo mengine atakagua na kuhamasisha zoezi la urasimishaji ambalo limeonekana kuwa na changamoto katika baadhi ya maeneo.

Vile vile, katika kuhakikisha migogoro ya ardhi inapungua nchini Lukuvi mwanzoni mwa mwezi Desemba atakuwa na ziara ndefu itakayohusisha mikoa ya Songwe, Mbeya, Njombe, Iringa na Pwani ambapo wananchi watapata fursa ya kuwasilisha kero za ardhi kupitia programu ya ‘Funguka kwa Waziri.’

Ziara hiyo ni muendelezo wa ziara zake za kushughulikia migogoro ya ardhi ikiwa ni baada ya kutoka mkoani Kilimanjaro ambapo alitatua migogoro ya ardhi ikiwemo ya mashamba makubwa katika Wilaya za Hai, Moshi na Same.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!