Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lukuvi amteua Polepole ujumbe Bodi ya NHC
Habari za Siasa

Lukuvi amteua Polepole ujumbe Bodi ya NHC

Spread the love

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameteua wajumbe saba wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), akiwemo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa kwa umma iliyotolewa tarehe 20 Mei 2019 na Lukuvi imewataja wajumbe hao wapya akiwemo, Immaculate Senje, Sauda Msemo, Martine Madekwe, Mhandisi Mwita Rubirya, Abdallah Mwinyimvua  na Charles Singili.

“Kwa mamlaka niliyopewa chini ya Aya ya 1 (1) (b) ya Jedwali lililoanzishwa chini ya kifungu cha 5(2) cha Sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa sura 295, nimewateua wajumbe wa bodi kuanzia leo tarehe 20 Mei 2019,” inaeleza taarifa ya Lukuvi.

Waziri Lukuvi amefanya uteuzi huo kufuatia uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa Dk. Sophia Kongela uliofanywa na Rais John Magufuli hivi karibuni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!