MFANYABIASHARA Said Lugumi ametelekeza agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Kangi Lugola liliomtaka ajisalimishe ofisini kwake mara moja. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Taarifa ya Jeshi la Polisi inaeleza kuwa, Lugumi asubuhi ya leo tarehe 31, Julai 2018 amewasili katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa ajili ya kuonana na Waziri Lugola.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa, kabla ya polisi kumpeleka Lugumi kwa Waziri Lugola, alipelekwa Makao Makuu ya Polisi Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai.
Waziri Lugola Julai 22, 2018 alimtaka Lugumi ajisalimishe ofisini kwake kabla ya Julai 31 mwaka huu.
Leave a comment