Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugola: Tutafika pahala, maiti zitachukuliwa hatua
Habari Mchanganyiko

Lugola: Tutafika pahala, maiti zitachukuliwa hatua

Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Spread the love

KANGI Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi amekemea uzembe wa baadhi ya askari polisi dhidi ya wahalifu wa ujambazi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lugola ameeleza kuwa, uzembe huo ukikithiri itafikia pahala mamlaka husika zitaanza kuchukulia hatua maiti, za askari polisi atakaye zembea katika kupambana na wahalifu wa ujambazi.

“ Jambazi ambaye anakutana na Polisi kabla hajajiandaa kuwawahi Polisi, tayari awe amewahiwa zamani na kuangushwa chini. Na ninasema, Polisi ambaye atazembea zembea mpaka akawahiwa wakati na yeye ana mashine yake, tutafika pahala hata maiti sasa tuanze kuichukulia hatua,” amesema Lugola.

Lugola amesema kushughulika na majambazi sio sawa na kutongoza mwanamke, na kwamba lazima Polisi wawahi majambazi kabla hawajadhuru wananchi au wao wenyewe.

“Kushughulika na majambazi sio sawa na tunavyotongoza mwanamke. Unajua dada nakumaindi, unajua dada ulinipa namba ya bajaji. Hakuna, nimesema jambazi ambaye anakwenda kufanya ujambazi awahiwe kabla ya huyo jambazi hajamuwahi mwananchi,” amesema Lugola.

ReplyForward

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!