Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugola awageukia wavamizi wa maeneo ya Majeshi
Habari Mchanganyiko

Lugola awageukia wavamizi wa maeneo ya Majeshi

Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaelekeza wakuu wote wa vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini kuainisha maeneo yote ya ardhi wanayomiliki ili kuepusha uvamizi wa maeneo hayo kwa baadhi ya wananchi na makampuni mbalimbali. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Lugola amesema kuwa ameagiza wakuu wa vyombo hivyo vya ulinzi kuainisha maeneo yaliyopimwa na yenye hati miliki na kuainisha maeneo ambayo yana migogoro na wananchi ama taasisi pamoja na hatua ambazo zimefikiwa katika kushughulikia migogoro hiyo.

“Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wananchi na makampuni mbalimbali kuvamia maeneo yanayomilikiwa na majeshi yaliyoko ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na kufanya shuguli mbalimbali za uzalishaji ikiwemo kilimo, ufugaji na hata kuanzisha viwanda, kuanzia leo ni marufuku kwa mwananchi, kampuni au shirika kuvamia maeneo yanayomilikiwa na vyombo vya Ulinzi na Usalama likiwemo Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji, Uhamiaji na mtu yoyote atakayebainika kufanya hvyo atachukuliwa hatua za kisheria,” amesema.

Katika hatua nyingine, Lugola ameagiza Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani kuweka utaratibu maalum wa kukamata magari hasa yakiwa na abiria kunakopelekea kuwachelewesha abiria hao katika shughuli zaidi huku wakiwa hawana hatia yoyote.

Lugola ameagiza kuwepo na utartibu wa kutokamatwa kwa magari yanapofanya makosa yakiwa na abiria badala yake yaachwe hadi yafike mwisho wa safari na yashushe abiria na ndio dereva akamatwe.

“Nimemuelekeza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini kuhakikisha jambo hili halitokei tena, kwa mfano leo nimepigiwa simu baadhi ya abiria wakilalamika kufanyiwa jambo hilo na askari aliyewakamata akawaacha kituoni na akaenda zake,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!