Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugola awageukia wavamizi wa maeneo ya Majeshi
Habari Mchanganyiko

Lugola awageukia wavamizi wa maeneo ya Majeshi

Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaelekeza wakuu wote wa vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini kuainisha maeneo yote ya ardhi wanayomiliki ili kuepusha uvamizi wa maeneo hayo kwa baadhi ya wananchi na makampuni mbalimbali. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Lugola amesema kuwa ameagiza wakuu wa vyombo hivyo vya ulinzi kuainisha maeneo yaliyopimwa na yenye hati miliki na kuainisha maeneo ambayo yana migogoro na wananchi ama taasisi pamoja na hatua ambazo zimefikiwa katika kushughulikia migogoro hiyo.

“Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wananchi na makampuni mbalimbali kuvamia maeneo yanayomilikiwa na majeshi yaliyoko ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na kufanya shuguli mbalimbali za uzalishaji ikiwemo kilimo, ufugaji na hata kuanzisha viwanda, kuanzia leo ni marufuku kwa mwananchi, kampuni au shirika kuvamia maeneo yanayomilikiwa na vyombo vya Ulinzi na Usalama likiwemo Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uokoaji, Uhamiaji na mtu yoyote atakayebainika kufanya hvyo atachukuliwa hatua za kisheria,” amesema.

Katika hatua nyingine, Lugola ameagiza Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani kuweka utaratibu maalum wa kukamata magari hasa yakiwa na abiria kunakopelekea kuwachelewesha abiria hao katika shughuli zaidi huku wakiwa hawana hatia yoyote.

Lugola ameagiza kuwepo na utartibu wa kutokamatwa kwa magari yanapofanya makosa yakiwa na abiria badala yake yaachwe hadi yafike mwisho wa safari na yashushe abiria na ndio dereva akamatwe.

“Nimemuelekeza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini kuhakikisha jambo hili halitokei tena, kwa mfano leo nimepigiwa simu baadhi ya abiria wakilalamika kufanyiwa jambo hilo na askari aliyewakamata akawaacha kituoni na akaenda zake,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!