Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugha ya Kichina yasababisha mgomo kampuni ya ujenzi
Habari Mchanganyiko

Lugha ya Kichina yasababisha mgomo kampuni ya ujenzi

Spread the love

MGOMO wa wafanyakazi zaidi ya 290 wa Kampuni ya Kimataifa ya Geo Engineering ya China inayotekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya Sanya Juu hadi  Elerai kwa kiwango cha lami umetikisa mkoa wa Kilimanjaro, anaandika Mwandishi Wetu.

Mkuu wa Wilaya ya Siha, Onesmo Buswelu amethibitisha kuwa wafanyakazi hao wamegoma wakilalamikia mikataba yao ya ajira kuandikwa kwa lugha ya Kichina na mingine kwa Kiingereza, badala ya Kiswahili.

Kufuatia hali hiyo, amelazimika kukutana na uongozi wa kampuni hiyo na wawakilishi wa wafanyakazi hao na kutoa maelekezo ya kurekebishwa kwa changamoto hizo, huku akiwasihi wafanyakazi kuendelea na kazi wakati suala hilo likitafutiwa ufumbuzi.

“Serikali tumeshakutana nao tayari na hao viongozi wa kampuni inayotekeleza mradi huo na kutoa maelekezo ya kurekebishwa kwa changamoto hiyo ya mikataba. Lakini pia tumewaonya wafanyakazi au mtu yeyote asithubutu kuwashawishi wafanyakazi wagome au kushinikiza kuungwa mkono, watakiona chamtemakuni,”amesisitiza.

Ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 32.2 za lami zinazojengwa kwa gharama ya Sh. bilioni 52.19 unatarajiwa kukamilika Oktoba 15, mwaka 2018.

Barabara hiyo inatajwa kuwa mkombozi kwa wananchi wa Wilaya ya Siha, kwa vile ndiyo injini ya kuchochea uchumi wa mkoa wa Kilimanjaro na inayoimarisha sekta ya uchukuzi na biashara kati ya mataifa ya Tanzania na Kenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!