Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugha tatizo utafiti wa kilimo cha umwagiliaji
Habari Mchanganyiko

Lugha tatizo utafiti wa kilimo cha umwagiliaji

Spread the love

WATAFITI kutoka Vyuo vikuu mbalimbali nchini wametakiwa kutafsiri tafiti zinazofanyika kwa lugha nyepesi ili kuweza kutumika na kutatua matatizo yanayopatikana kwenye maeneo mbalimbali kila wakati ikiwemo changamoto ya matumizi ya maji kiholela katika kilimo cha umwagiliaji iliyopo kwa sasa. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Rasilimali za maji, Praxeda Karugendo alisema hayo jana wakati akizindua kitabu cha mwongozo wa kutathmini ubora na afya ya mto kwa njia ya TARISS fupi kilichoandaliwa na bodi ya maji bonde la Rufiji chenye malengo ya kufuatilia ubora wa maji kwa kutumia wadudu ambao ni viumbe hai ili kuhimili uharibifu wa mazingira ya mto na maji kwa ujumla.

Karugendo alisema kuwa ikiwa tafiti zinazofanyika zikiendelea kutafsiriwa kama ilivyokuwa hii ya kufuatilia ubora wa maji itasaidia pia katika matumizi ya maji katika kilimo cha umwagiliaji ambayo yapo kiholela.

“kwa sasa mnatafsiri kwa lugha rahisi na zinatumika,  hivyo nimefurahi sana kwa kuwa tumepata mahali pakuanzia, uwe ni mwanzo wa kushawishi tafiti zingine ambazo bado hazijatumika ipasavyo ikiwemo eneo la umwagiliaji na matumizi ya maji lipo vibaya” alisema Karugendo.

Alisema, katika mabonde mengi ya umwagiliaji Tanzania maji yanaonekana hayatoshi kutokana na njia zinazotumika katika umwagiliaji kuwa zipo kiholela.

Aidha Karugendo alisema, Tanzania ina vyanzo vingi vya maji vyenye changamoto nyingi kwa aliipongeza Wizara ya maji na Umwagiliaji kwa sasa kuona umuhimu wa kubuni muundo wa kusimamia maji kutokana na sera ya maji.

Hivyo aliwataka viongozi wa Jumuiya za wamiaji maji kujiona kuwa wao bado ni watu muhimu katika kuhakikisha vyanzo vya maji vinatunzwa.

Naye Mwenyekiti wa Mradi wa Shahidi wa maji, Herbert Kashililah alisema, rasilimali za maji zinaanza kuwa ni tishio ingawa watanzania wanaona tunayo mengi sana kwani kiwango cha maji kimeonekana kupungua na kuwa chini ya 1700 hadi 1800.

Alisema kiwango hicho kikizidi chini ya 1700 tunaanza kuingia kwenye mfumo wa uhaba wa maji na kuanza kupigana kutafuta maji.

“tusifike huko kwa kuwa wakimbizi wa kimazingira, watu wanaokimbia kutokana na athari zinazotokana na uharibifu wa kimazingira ikiwemo maji na maji ndio itakuwa sehemu ambayo sisi tutagombana” alisema.

Kashililah alisema, Tanzania ya Viwanda haiwezi kuanza peke yake hivi hivi kama hawataanza kulima ambapo dhana ya TARISSfupi iliyozinduliwa leo itakuwa na changamoto sana wakati huo kama viwanda vikiwa vingi watu wakilima sana kwa viatilifu na kumwaga kwenye mito na hivyo vimelea vya vidudu hai havitaweza kuonekana kabisa.

Hivyo alisema, ni vema wakaanza kufikiria mbali kwa kujiandaa na matokeo hayo ambapo alisema usimamiaji wa rasilimali za maji sio wa Taasisi ya bonde la mto rufiji pekee ni wetu sote ambapo tushirikiane na kuziwezesha Jumuiya za watumiaji maji kuwa mbele katika kusimamia maji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!