Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lowassa aitosa Chadema, arudi CCM
Habari za SiasaTangulizi

Lowassa aitosa Chadema, arudi CCM

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM akimpokea Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliporejea CCM
Spread the love

WAZIRI Mkuu Mstaafu wa serikali ya awamu ya nne, Edward Lowassa amerejea CCM akitokea Chadema. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Lowassa amerejea CCM leo tarehe 1 Machi 2019 na kupokelewa na Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Bashiru Ally katika ofisi ndogo za CCM jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kumpokea Lowassa, Dk. Bashiru ameeleza kuwa ujio wa mwanasiasa huyo mkongwe hapa nchini unaashiria kwamba chama hicho kinaanza kazi ya kujenga Taifa.

“Kama alivyosema Waziri Mkuu Mstaafu Lowasa amerudi nyumbani, tunaanza kazi ya kujenga taifa letu na kulinda udugu wetu ,” amesema Dk. Bashiru.

Lowassa alihama CCM katika vuguvugu la kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 baada ya kushindwa katika kura za maoni za kuwania nafasi ya kuipeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa urais, na kuipata fursa hiyo kupitia Chadema kwa mwamvuli wa vyama vinavyounda UKAWA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!