Wednesday , 17 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Wataiba kura zangu
Habari za Siasa

Lissu: Wataiba kura zangu

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amedai ushindi wake ukiwa mwembamba, ‘utapinduliwa.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Muleba … (endelea).

Amesema, kukabiliana na hilo, amewataka Watanzania kumpigia kura kwa wingi ili wapinduaji wakose mahala pa kuanzia.

“Tukishinda kwa ushindi kidogo, wale wataiba na pia tukishinda kawaida, wataiba. Sasa ili wasiibe, inatubidi tushinde kwa kura nyingi.

“Tushinde kwa kura za kimbunga ili wakose sehemu ya kuanzia kupindua. Inabidi wakute kila kituo cha kuhesabia kura kwenye jimbo, wilaya, mkoa tumeshinda,” amesema.

Mgombea huyo ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa chama hicho ametoa kauli hiyo tarehe 23 Septemba 2020, kwenye kampeni zake za urais akiwa Kamachumu, Muleba mkoani Kagera.

Amesema, njia rahisi ya kuzuia kile alichoita ‘balaa’ kisitokee, ni wananchi kujitokeza kupiga kura kwa wingi tarehe 28 Oktoba 2020.

“Mwezi ujao tuzuie hili balaa, tupige kura tujikomboe,” amesema Lissu akisisitiza, kwamba kwa kufanya hivyo, itakuwa ni ukombozi kwa Taifa.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!