Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa LISSU: Tutashinda kwa asilimia 65 hadi 75
Habari za SiasaTangulizi

LISSU: Tutashinda kwa asilimia 65 hadi 75

Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema amesema, wamefanya utafiti wa kuangalia mwitikio wa wananchi kwenye mikutano yao, upigaji kura na kubaini katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 watashinda urais kwa asilimia 65 hadi 75. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi…(endelea)

Lissu amesema hayo leo asubuhi Jumamosi tarehe 24 Oktoba 2020 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuendelea na ratiba yake ya mikutano ya kampeni majimbo ya Tunduru, Nyasa na Songea Mkoa wa Ruvuma.

Amesema, tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi huo tarehe 26 Agosti 2020, tumefanya mikutano mingi ya kampeni kuliko mshindani wangu mkuu Rais John Magufuli (wa CCM), kuliko hata mgombea wake mwenza (Samia Suluhu Hassan) au waziri mkuu (Kassim Majaliwa).”

“Hakuna mkutano ambao imebidi tusafirishe mtu yoyote, ni waliokuja kwa kutembea wao wenyewe, usafiri wanaoujua wao, yaani kwa kujitegemea. Mikutamno yao ya Rais Magufuli, mgombea mwenza au waziri mkuu wanabeba watu ili kujaza,” amesema Lissu

Amesema, wamewatumia wataalamu kufanya utafiti maeneo mbalimbali nchini juu ya upigaji kura na, “wataalamu wetu wa mahesabu wanaofuatilia na kufanya utafiti, jinsi ya tulivyofanya mukutano, mwelekeo wa uchaguzi ni kwamba tunashinda uchaguzi huu kati ya asilimia 65 hadi 75.”

Lissu ametumia fursa hiyo kuwaomba, wananchi katika siku hizi tatu zilizosalia kuwa makini hususan mawakala ili kutofanyiwa mchezo mchafu wa kisiasa utakaowawezesha washindani wao kutumia mwanya huo.

Mgombea huyo wa Urais amesema, wamepokea hivi karibuni daftari wa wapiga kura na wanaendelea kulichambua ili kubaini wapiga kura na vituo kama vipo hewa na siku chache zijazo, watazungumza na waandishi wa habari juu ya kile watakachokuwa wamekibaini.

“Wataalamu wetu wanaendelea kulifanyia kazi kwa kulichambua na taarifa itatoka kabla ya Jumatatu. Wameandika majina ya watoto na tumeona wanafunzi wanafundishwa kupiga kura wakiwa darasani na mgombea mmoja wa ubunge wa CCM.”

“Watu wetu ndani ya CCM, tume na huko mitaani wanatupa taarifa za kutosha juu ya baadhi ya hujumu zinazoweza kufanywa,” amesema

Lissu amesema “mara nyingi nimesema na ninarudia tena, wakitaka kuharibu uchaguzi, wanataka kupelekwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), kuna uchunguzi umekwisha kuanza kwa yaliyofanyika na yatakayofanyika, hivyo niwaonye, wanaotaka kuuharibu uchaguzi huu, wasifanye hivyo.”

Amesema, tayari kuna orodha ya watu imekwisha kuanza kuwafuatilia “yeyote atakayetumia mbinu za kiharimia kuharibu uchaguzi, anajiingiza mwenyewe kwenye orodha ya ICC, kama wanafikiri watavuruga uchaguzi, yakatokea maafa halafu wakabaki salama, wanajisahau.”

Lissu ametoa wito kwa “wakuu wa vikosi, wakuu wa majeshi yetu, nawaombeni, nawasihi, kumbukeni viapo vyetu kwamba ninyi ni wanajeshi wa wananchi, msitumie silaha zenu dhidi ya sisi wananchi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!