Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Narejea Tanzania kabla ya Julai 28
Habari za SiasaTangulizi

Lissu: Narejea Tanzania kabla ya Julai 28

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

TUNDU Antipas Lissu, Makamu mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema, atarejea Tanzania mwishoni mwa mwezi huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, atafanya hivyo ili aweze kuhudhuria mkutano wa Baraza Kuu na mkutano mkuu wa chama hicho tarehe 28 na 29 Julai 2020.

Mikutano hiyo, pamoja na mambo mengine, itampitisha mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020.

Mchakato wa uchakuaji na urejeshaji fomu za kuwania Urais wa Tanzania unaanza leo Jumamosi tarehe 4 hadi 19,2020.

Wagombea au mawakala wao watakuwa na fursa ya kuchukua fomu kisha kutafuta wadhamini 100 katika kila kanda kumi za chama hicho.

Lissu ni miongoni mwa wanachama ambao wamekwisha tia nia hadharani ya kuwania nafasi hiyo ya juu kabisa ya uongozi wa Taifa hilo lililopo Afrika Mashariki.

Akijojiwa na mwandishi nguli nchini Tanzania, Jenerali Ulimwengu katika kipindi chake kinachorushwa na JeneraliOnline, Lissu amesema, baada ya safari ndefu ya kutibu majeraha na kupona, sasa yuko tayari kurejea nchini humo.

Amesema anarejea ili kuomba ridhaa ya wana Chadema na Watanzania kumchagua kuwa Rais wa Tanzania ili kuwatumikia kwa kuunganisha nguvu kwa pamoja kwani ana imani mtu mmoja pekee hawezi kuongoza nchini.

Tangu tarehe 7 Septemba 2017, Lissu aliposhambuliwa na watu wasiofahamika akiwa nyumbani kwake Area D jijini Dodoma, mwanasiasa huyo amekuwa nje ya Tanzania kwa matibabu.

Siku hiyohiyo usiku, alihamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya kwa matibabu hadi tarehe 6 Januari 2018 alipopelekwa nchini Ubelgiji kwa matibabu zaidi.

Hata hivyo, Lissu mwenyewe amekwisha kusema amepona na hatumii dawa zozote na anachosubiri ni kureja nyumbani Tanzania kuendelea na shughuli zake mbalimbali hasa za kisiasa.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!