WANACHAMA na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), watamsindikiza Tundu Lissu kwa maandamano kutokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere hadi Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni, Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu tarehe 27 Julai 2020 na Hemed Ally, Katibu wa Chadema Kanda ya Pwani, akizungumza na wanahabari uwanjani hapo.
Lissu alikuwa nje ya nchi kwa takribani miaka mitatu kwa ajili ya matibabu, baada ya kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana, tarehe 7 Septemba 2020, jijini Dodoma.
Hemed amesema, wafuasi wa Chadema wameamua kumsindikiza Lissu kwa maandamano hadi makao makuu ya chama hicho, ikiwa ni sehemu ya kuonyesha furaha yao juu ya ujio wa kiongozi huyo.
“Ni haki yetu kumpokea Lissu na tutamsindikiza kwa maandamano hadi makao makuu ya chama. Polisi wanatekeleza wajibu wao lakini na sisi ni haki yetu kumpokea kiongozi wetu aliyekuwa nje ya nchi kwa muda mrefu,” amesema Hemed.
Awali, kundi la wafuasi wa Chadema walizuiliwa kuingia uwanjani hapo, lakini baadae polisi waliwaruhusu waingie ndani.
Tayari Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema na John Mnyika, Katibu Mkuu wa chama hicho wapo uwanjani hapo.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari zaidi
Leave a comment