Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu azua kizazaa mahakamani Dodoma
Habari za Siasa

Lissu azua kizazaa mahakamani Dodoma

Kulia: Tundu Lissu akiondoka mahakamani baada ya kuhakikishia na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa (picha ya kushoto).
Spread the love

MWANASHERIA wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu leo ametumia zaidi ya saa nne akiwa katika mahakama ya wilaya Dodoma akigoma kutoka humo akihofia kukamatwa, anaandika Dany Tibason.

Lissu akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma amesema jana majira ya asubuhi mke wake alimpigia simu na kumueleza kuwa askari kanzu wapatao sita walifika nyumbani kwake Dar es salaam wakimtafuta.

Hata hivyo, Lissu amesema akiwa mjini Dodoma akiendelea na kesi ya walimu ambao ni wateja wake alipokea taarifa kuwa wapo askari nje ya mahakama wanamsubiri wamkamate.

Kutokana na taarifa hiyo Lissu aligoma kutoka mahakamani hapo hatua ambayo ilisababisha kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa kwenda kumuona na kumhakikisha kwamba hakuna mtu anayemtafuta.

Kauli hiyo ya Mambosasa ilimpa uhakika Lissu na hivyo kuamua kutoka nje ya Mahakama na kuendelea na shughuli zake.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!