MSAFARA wa Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema umelazimika kutumia mtubwi kutoka Kisorya mkoani Mara kwenda Ukerewe Mkoa wa Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea)
Leo Jumatano tarehe 14 Oktoba 2020, msafara wa Lissu walifika eneo hilo la Kisorya ili kwenda Ukerewe umbali unaokadiliwa kuwa kilomita 21.9 kuhutubia mkutano wa kampeni lakini, kivuko kinachotoa huduma eneo hilo kilielezwa ni kibovu.
Kwa mujibu wa rariba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inaonyesha mkutano wa kwanza Lissu anapaswa kuufanya Ukerewe kisha baadaye atakuwa Jimbo la Rorya Mkoa wa Mara.
Katika ukurasa wake wa Twitter, Lissu ameweka video wakiwa wanataka kuanza safari na kuandika “kwa mara ya pili katika kipindi hiki cha kampeni, bila sababu za msingi, hamna kivuko cha Kisorya kwa ajili ya msafara wetu kwenda Ukerewe.”
“Yote ni kwa ajili ya kuzuia tusifike huko. Sasa tutavuka kivingine na tutafanya mkutano kama ilivyo ratiba! Haturudi nyuma,” amesema Lissu.
Leave a comment