Friday , 29 March 2024
Habari za SiasaTangulizi

Lissu atoa ya moyoni

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge was Singida Mashariki amesema kuwa upinzani umeshambuliwa kuliko kipindi chochote nchini Tanzania. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Lissu amesema hivyo leo tarehe 28 Agosti 2018 usiku saa 3:23 alipozungumza katika kipindi cha BBC Swahili.

Mbunge huyo aliyepigwa risasi mjini Dodoma yapata mwaka mmoja uliopita amesema katika kipindi cha miaka miwili ya sasa, upinzani umeshambuliwa kwa kiwango kikubwa.

Alisema hivyo baada ya kuulizwa swali na mtangazaji Zuhura Yunus kwamba, upinzani umelegalega nchini Tanzania.

Alijibu swali hilo Lissu amesema, itakua ajabu kama upinzani utabaki vile katika kipindi hiki.

“Wapinzania hawajanyamaza, ila umeshambuliwa,” amesema Lissu na kuongeza “ni ajabu kama tungeendelea kuwa kama wa Kikwete (Rais Kikwete, Rais Mkapa).

Pia Lissu amesema kuwa, Bunge lilitoa taarifa ya kukataa kumlipia matibabu kwa madai ya kutofuata utaratibu.

Amesema, atapona vizuri atarejea nchini huku akiwa na tahadhari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!