MWANASHERIA Mkuu wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (Chadema) ameikosoa serikali kuhusu namna inavyoshughulikia suala la uchochezi katika serikali ya awamu ya tano, anaandika Victoria Chance.
Akiongea na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya Chadema Kinondoni Jijini Dar Es Salaam Lissu ameorodhesha matukio mbalimbali ambayo serikali inadai kuwa ni ya uchochezi, orodha ambayo Lissu anaipinga.
Alianza kwa kuelezea kwamba kuna utaratibu unaondaliwa ili kumfikisha Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa mahakamani kwa kosa la uchochezi kama ambavyo mwalimu Julius Kambarage Nyerere alishtakiwa enzi za ukoloni wakati hakuwa na hatia.
Aidha Lissu alieleza kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Vicent Mashinji, aliwekwa ndani kwa sababu hiyo hiyo ya uchochezi. Tayari Dk. Mashinji amepewa dhamana ya polisi huko Mbamba Bay, mooani Ruvuma, alikokuwa amekamatiwa na polisi.
Lissu ameongezea kuwa, “Wabunge wetu kadhaa akiwemo Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea, amabao either (ama) wamekamatwa au kushtakiwa kwa makosa yanayofanana na hayo.”
Aliendelea, “Na kuna wanacahama zaidi ya 51 wa Wilaya ya Chato wamekatwa kwa sababu ya kufanya kikao cha ndani wakati dikteta uchwara akiwa likizo.”
Pia aliendelea kuelezea kuwa kuna mamia ya watu wamewekwa ndani kwa kosa la kutumia simu zao kutuma ujumbe wa maandishi ambao haumpendezi Rais Magufuli na wapambe zake.
Kadhalika, alisema kuwa mnamo tarehe 29 Juni mwaka jana yeye mwenyewe alishtakiwa kwa kosa hilo hilo la uchochezi.
Kutokana na hayo Lissu amemalizia kwa kusema kwamba, “Rais Magufuli anatakiwa kupingwa na ajue kwamba nchi hii inakatiba, na kwamba, wale watakao muunga mkono katika haya ni dhahiri watakuwa hawana akili.”
Lissue amawahimiza Watanzania kipaza sauti zao kwani mahali tulipofikishwa sio salama kisiasa.
Leave a comment