Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu akumbana na kikwazo Chato
Habari za Siasa

Lissu akumbana na kikwazo Chato

Tundu Lissu
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amekumbana na kituko cha kwanza Chato mkoani Geita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato … (endelea).

Taarifa kutoka Chato zinaeleza, usiku wa kuamkia leo Jumanne tarehe 13 Oktoba 2020, eneo la biashara la Masai  Machae, mgombea ubunge kupitia chama hicho katika jimbo hilo, limevamiwa na kuvunjwa.

Lissu kwenye ukurasa wake wa twitter amesema, licha ya uvamizi na vitisho hivyo, mkutano wake wa kampeni aliopanga kuufanya leo, utatekelezwa bila hofu yoyote.

“Leo ni siku ya mkutano wetu Jimbo la Chato na tayari wameanza kutufanyia fujo. Usiku wa kuamkia leo wamevamia biashara ya Mgombea ubunge wetu na nyumba ya Katibu wa Jimbo na kuharibu mali zao. Hatutishiki na hatutatishika. Mkutano wetu wa Chato uko pale pale,” amesema Lissu.

Mgombea huyo ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Chadema, anamalizia kampeni zake katika Mkoa wa Shinyanga na leo atafanya kampeni majimbo ya Bukombe, Mbogwe na mkutano wa mwisho utakuwa Chato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!