Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu ajigamba ‘sipoi’
Habari za Siasa

Lissu ajigamba ‘sipoi’

Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema licha ya Ofisi ya Kanda ya Kaskazini kuchomwa moto, ratiba yake ya leo haibadiliki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Taarifa kutoka Arusha zinaeleza, usiku wa kuamkia leo tarehe 14 Agosti 2020, Ofisi za Chadema kanda hiyo zimeshambuliwa na kuteketea kwa moto.

Jeshi la Polisi jijini Arusha limeeleza kuendelea na uchunguzi na kisha kutoa taarifa ya nini kilichotokea.

Kwenye ukurasa wake wa twitter, Lissu ameandika kwamba, tayari ameingia kwenye jiji hilo kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili kukamilisha utaratibu wa Tume ya Uchaguzi (NEC) ya kupata wadhamini wa urais kutoka kila mkoa.

Hata hivo ameeleza, pamoja na tukio hilo baya kutokea akiwa ndio ameingia kwenye mkoa huo, tukio la shambulizi kwenye ofisi hizo halitikisi kile alichokusudia kufanya leo.

“Ofisi zetu za chama za Kanda ya Kaskazini zilizopo Arusha zimeshambuliwa na kuharibiwa wakati nikiingia Arusha. Ratiba ya leo itabaki vile vile. Hakuna kiwango chochote cha hofu kinaweza kuzuia mabadiliko haya ya sunami Tanzania,” amesema.

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!