Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu agoma kula, ashinikiza kupelekwa mahakamani
Habari za Siasa

Lissu agoma kula, ashinikiza kupelekwa mahakamani

Wakili Peter KIbatala (kushoto) akijadili jambo na mteja wake, Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, amegoma kula chakula kutwa nzima ya leo, akishinikiza kupeleka mahakamani, anaandika Faki Sosi.

Kwa mujibu wa wakili wa Lissu, Peter Kibatala, mteja wake amegoma kula toka asubuhi, mchana na jioni kwa madai hata fanya hivyo mpaka atakapopelekwa mahakamani.

“Mke wa Lissu alileta chakula asubuhi, lakini Lissu aligoma kula na kumwambia mkewe asihangaike kwani hatakuka mpaka atakapofikishwa mahakamani,” amesema Kibatala.

Kibatala amesema kwa sasa wanapigania mteja wake apelekwe mahakamani kwani muda wa kisheria kushikiriwa kituoni umemalizika.

Lissu alikamatwa jijini Dodoma nje ya viwanja vya Bunge, Februari 6, 2017 na kuletwa Dar es Salaam katika kituo cha Polisi cha Kati kwa mahojiano, huku kosa lake likidaiwa ni kauli za uchochezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!