Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Ligi Kuu VPL kurejea tena leo
Michezo

Ligi Kuu VPL kurejea tena leo

Uhefu FC
Spread the love

LIGI kuu soka Tanzania Bara inaendelea tena leo kwa kupigwa jumla ya michezo minne katika viwanja tofauti mara baada ya mapumziko ya michezo ya kirafiki na kimashindano ya kalenda ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani ‘Fifa.’ Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo wa mapema leo utawakutanisha JKT Tanzania ambao watakuwa nyumbani dhidi ya Ruvu Shooting, mechi itakayochezwa majira ya saa 8 mchana kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Mechi nyingine tatu zitachezwa majira ya saa 10 kamili jioni, ambapo KMC watawakaribisha Coastal Union kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam na Biashara United atakuwa kwenye dimba la Karume mkoni Mara kuwaalika Ihefu FC kutoka Mbeya.

KMC

Baada ya kupoteza dhidi ya Azam FC, klabu ya Kagera Sugar itakuwa na wakati wa kujiuliza mbele ya Namungo FC kwenye mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Majaliwa, Luangwa mkoani Lindi.

Mpaka ligi hiyo inasimama Azam FC walikuwa juu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 15 huku nafasi ya pili ikishikwa na Simba yenye pointi 13 sawa na Yanga aliyeshika nafasi ya tatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!