SERIKALI ya Hispania kupitia Waziri Mkuu wake Pedro Sanchez, ametangaza kuwa Ligi Kuu Hispania ‘La Liga’ itarejea tena Juni 8, 2020 baada ya kusimama kwa mwezi mmoja kutokana na kuibuka kwa janga la Corona. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Sanchez amesema kuwa tayari nchi hiyo imeshafanya kila kitu kulichopaswa kufanya na hivyo na muda utafika wa kurudisha shughuli za watu za kila siku huku akitangaza tarehe rasmi ya kuendelea kwa ligi hiyo.
Tayari wachezaji mbalimbali wamesharipoti kwenye klabu zao na kuunza mazoezi kwa makundi katika chukua tahadhali kama zilizo hainishwa na mamlaka ya afya nchini humo.
Ligi hiyo ambayo ilisimama Machi 23, 2020 baada ya mlipuko wa ugonjwa wa Covid 19, ikiwa imeshachezwa michezo 27 kwa kila timu huku klabu ya Barcelona ikiwa kileleni kwa alama 58 tofauti ya alama mbili tu na wapinzania wao Real Madrid ambao wana alama 56.
Leave a comment