Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa LHRC yafichua madudu mengine
Habari za SiasaTangulizi

LHRC yafichua madudu mengine

Spread the love

MATOKEO ya ripoti ya Haki za Binadamu na Biashara ya mwaka 2017 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) yamebainisha kwamba kutoshirikiswa kwa wananchi katika mchakato wa utwaaji ardhi kwa ajili ya uwekezaji kumepelekea uwepo wa migogoro ya ardhi katika baadhi ya maeneo hapa nchini. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea) .

Akielezea matokeo ya Ripoti hiyo iliyozinduliwa leo tarehe 16 Agosti, 2018 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Wakili Anna Henga, Mratibu Msaidizi wa Haki za Binadamu na Biashara, Tito Magoti amesema wawekezaji wengi huchukua maeneo makubwa pasina kuyatumia kitendo kinachosababisha wananchi kuanzisha migogoro.

Wakili Magoti ametaja baadhi ya mikoa yenye migogoro hiyo ikiwemo mkoa wa Manyara, Kilimanjaro hasa Wilayani Moshi na Musoma ambapo utafiti wao ulibaini kwamba wawekezaji wengi hawayatumii maeneo kitendo kinachonyima fursa wananchi wa eneo husika kuyatumia.

“Wawekezaji hupewa maeneo makubwa huku wananchi wakizuiwa kutumia maeneo wanayoshindwa kuyatumia. Vile vile utafiti umebaini kwamba wananchi hawashirikishwi katika mchakato wa ugawaji wa ardhi kwa wawekezaji kitendo kinacholeta migogoro,” amesema Magoti.

Kufuatia matokeo hayo, Magoti ameitaka serikali hasa serikali za mitaa kuwashirikisha wananchi wakati wa mchakato wa utwaaji ardhi kwa ajili ya uwekezaji ili kuondoa migogoro isiyo na lazima.

Kuhusu matokeo ya ripoti hiyo, yamebainisha kwamba asilimia 64 ya wanajamii walioshiriki katika utafiti huo walidai kwamba wawekezaji hawakuwaruhusu wanakijiji kutumia sehemu ya ardhi hiyo kwa ajili ya shughuli za kiuchumi wakati asilimia 8 walikiri kuruhusiwa huku asilimia 28 wakisema hawajui.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!