Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Leo kila mwathirika MV Nyerere kulamba Mil 1
Habari za SiasaTangulizi

Leo kila mwathirika MV Nyerere kulamba Mil 1

Spread the love

RAIS John Magufuli anatarajiwa kutoa kiasi cha Shiling milioni moja kwa kila mwathirika wa ajali ya MV Nyerere iliyotokea tarehe 20 Septemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana na Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano.

Fedha hizo ni nje ya zile Sh. 500,000 zilizokabidhiwa kwa kila maiti ambapo fedha za leo zitaelekezwa kwa waliofiwa na walionusurika.

“Rais ameniagiza kuwa, ataongeza fedha kwa waathirika na atatoa shilingi milioni moja kwa waathirika wote waliopoteza ndugu zao na walionusurika,” amesema.

Amesema, idadi ya watu waliofariki imeendelea kuongezeka ambapo mpaka kufikia Jumatatu jioni maiti mbili ziliopolewa.

Na kwamba, wahusani wameendelea kuchanga fedha kwa ajili ya msaada kwa waathirika ambapo mpaka Jumatatu jioni likuwa zimeishakusanywa jumla ya Sh. 397 milioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!