GODBLESS Lema, Mbunge wa Arusha ametakiwa kufika Polisi Arusha leo tarehe 21 Oktoba 2018 kabla hakujakucha. Anaripoti Mariam Seleman … (endelea).
Mpaka sasa wito wa Lema kutoka Kituo Kikuu cha Polisi Arusha haujafahamika lengo lake.
Mbunge huyo ameandika kwenye ukurasa wake wa Tweeter kwamba, anaelekea Arusha kutekeleza wito huo.
“Nimepigiwa simu na Polisi kwamba natakiwa kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi Arusha leo bila kukosa, sijaelewa sababu lakini wito unaonekana kuwa wa lazima sana, lakini nafikiria kupigania haki hili ndio linaweza kuwa kosa langu kubwa. Msiogope.”
Nimepigiwa simu na Polisi kwamba natakiwa kuripoti kituo kikuu cha Polisi Arusha leo bila kukosa,sijaelezwa sababu lakini wito unaonekana kuwa wa lazima sana,lakini nafikiri kupigania haki ndio linaweza kuwa kosa langu kubwa. MSIOGOPE.
— Godbless E.J. Lema (@godbless_lema) October 21, 2018
Mpaka sasa hakujawa na taarifa mpya kutokana na wito huo.
Leave a comment