Friday , 19 April 2024
Habari za Siasa

Lema asakwa Dar

Godbless Lema, Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema)
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linadaiwa kuzingira Hoteli ya Regency Park iliyoko Mikocheni, jijini Dar es Salaam likimsaka Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Lema kupitia ukurasa wake wa twitter leo tarehe 17 Machi 2020, ameandika kwamba, polisi kadhaa waliovaa kiraia wamezingira hoteli hiyo.

“Polisi wengi wakiwa na magari wamevamia Hotel ninayo fikia Regency Park Mikocheni, nimepata taarifa kuwa wananitafuta,” ameandika Lema.

Chadema katika ukurasa wake wa twitter kimeeleza kwamba, hadi sasa hakijafahamu sababu za mbunge wake kusakwa na polisi.

https://twitter.com/godbless_lema/status/1239793753604395009

Na kwamba, Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, alipanga kufanya mkutano na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, kujibu kauli ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, DPP Biswalo Mganga, kwamba atamfungulia kesi kutokana na kutoa taarifa za uongoz juu ya Jeshi la Polisi mkoani Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!