Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Lampard astaafu soka
Michezo

Lampard astaafu soka

Frank Lampard
Spread the love

KIUNGO wa zamani wa klabu ya Chelsea, New York City FC na timu ya taifa ya England, Frank Lampard (38) leo ametangaza kustaafu mchezo wa mpira wa miguu baada ya kuucheza kwa mafanikio katika kipindi cha miaka 21, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Lampard ambaye mpaka anatangaza kustaafu soka ameshinda mataji matatu ya Ligi Kuu England, mataji mawili ya Kombe la Ligi, mataji matatu ya kombe la chama cha soka nchini England (FA) na taji la Klabu Bingwa Ulaya mara moja.

Mkongwe huyo ametangaza uamuzi wake wa kustaafu soka kupitia kwenye ukurasa wake unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram baada ya kuandika waraka mrefu kwenda kwa washabiki zake na wapenzi wa soka wote ulimwenguni.

Lampard aliandika kuwa huu ndio wakati sahihi wa yeye kustaafu mpira licha ya kupokea ofa nyingi ili aendelee kucheza mpira.

“Baada ya miaka 21 ya kucheza mchezo wa soka, sasa nimeamua kwamba ni wajati muafaka wa kustaafu mpira kama mchezaji wa kulipwa.”

“Wakati huo nimepokea ofa nyingi na nzuri kutoka nyumbani na nje ya nchi ili niendelee kucheza mpira, lakini kwa umri huu wa miaka 38 najisikia sasa ni wakati wa kuanza sura mpya katika maisha yangu,” aliandika Lampard kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mpanga anatangaza kutundika daruga, Lampard amecheza jumla ya michezo 106 katika timu ya taifa, na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu ya Chelsea baada ya kufunga mabao 211 kwa mashindano yote aliocheza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

error: Content is protected !!