Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Laini za simu kuzimwa Desemba 31
Habari Mchanganyiko

Laini za simu kuzimwa Desemba 31

Spread the love

WATU ambao hawatasajili laini zao za simu kwa alama za vidole, hawatoweza kuzitumia baada ya tarehe 31 Desemba 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Atashasta Nditiye, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ametoa kauli hiyo bungeni na kwamba, usajili wa laini za mitandao yote ya simu nchini, umepangwa kuanza tarehe 1 Mei 2019.

Amefafanua kwamba, baada ya kuanza kwa zoezi hilo, serikali itafanya mapitio yake mwezi Septemba ili kuona hatua iliyofikiwa, huku lengo la kuzima laini ambazo hazitakuwa zimesajiliwa likiwekwa kuwa tarehe ya mwisho wa mwaka huu.

“Zoezi la usajili litaanza tarehe Mosi Mei na tutafanya review (mapitio) mwezi wa tisa ili kuona ni watu wangapi wamekwishasajiliwa lakini mwisho kabisa itakuwa tarehe 31 Desemba mwaka huu,” amesema Nditiye.

Amesema kuwa, takwimu walizonazo kupitia Malaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ni kuwa, Watanzania walio na vitambulisho vya uraia wamefika milioni 16.

Nditiyealitoa ufafanuzi huo baada ya Felista Bura, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) kutaka kujua kuhusu malalamiko ya wananchi wengi ambao hawajapata vitambulisho hivyo, huku wakiwa na wasiwasi kwamba inawezekana laini zao zikafungwa kutokana na kutopata vitambulisho vya taifa.

Akifafanua zaidi Nditiye amesema, kampuni zote za simu nchini zimeelezwa kuanza kufanya usajili huo kwa njia ya lama za vidole, ikiwa ni baada ya kujiridhisha na utambuzi wa mtu kupitia kitambulisho cha uraia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!