Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Laini za simu kuzimwa Desemba 31
Habari Mchanganyiko

Laini za simu kuzimwa Desemba 31

Spread the love

WATU ambao hawatasajili laini zao za simu kwa alama za vidole, hawatoweza kuzitumia baada ya tarehe 31 Desemba 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Atashasta Nditiye, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ametoa kauli hiyo bungeni na kwamba, usajili wa laini za mitandao yote ya simu nchini, umepangwa kuanza tarehe 1 Mei 2019.

Amefafanua kwamba, baada ya kuanza kwa zoezi hilo, serikali itafanya mapitio yake mwezi Septemba ili kuona hatua iliyofikiwa, huku lengo la kuzima laini ambazo hazitakuwa zimesajiliwa likiwekwa kuwa tarehe ya mwisho wa mwaka huu.

“Zoezi la usajili litaanza tarehe Mosi Mei na tutafanya review (mapitio) mwezi wa tisa ili kuona ni watu wangapi wamekwishasajiliwa lakini mwisho kabisa itakuwa tarehe 31 Desemba mwaka huu,” amesema Nditiye.

Amesema kuwa, takwimu walizonazo kupitia Malaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ni kuwa, Watanzania walio na vitambulisho vya uraia wamefika milioni 16.

Nditiyealitoa ufafanuzi huo baada ya Felista Bura, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) kutaka kujua kuhusu malalamiko ya wananchi wengi ambao hawajapata vitambulisho hivyo, huku wakiwa na wasiwasi kwamba inawezekana laini zao zikafungwa kutokana na kutopata vitambulisho vya taifa.

Akifafanua zaidi Nditiye amesema, kampuni zote za simu nchini zimeelezwa kuanza kufanya usajili huo kwa njia ya lama za vidole, ikiwa ni baada ya kujiridhisha na utambuzi wa mtu kupitia kitambulisho cha uraia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!