Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Kuwaona Makambo, Kagere buku saba
Michezo

Kuwaona Makambo, Kagere buku saba

Spread the love
KUWAONA washambuliaji wawili Meddie Kagere wa Simba na Heritier Makambo wa Yanga wawili hao wataonyeshana ubabe Septemba 30, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa kiingilio cha Sh. 7000 tu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kagere amefunga mabao matatu katika Ligi Kuu akiwa anaongoza orodha ya wafungaji baada ya kucheza mechi tatu wakati Makambo amefunga bao moja katika mchezo mmoja aliocheza.

Uhodari washambuliaji hao ndiyo unaofanya mchezo wa watani wa jadi Simba na Yanga Septemba 30 kuwa na mzuka wa aina yake.

Mechi hiyo huteka hisia za wadau wengi wa soka kutokana na namna timu hizo mbili kuwa na ushindani pamoja na idadi kubwa ya mashabiki.

Katika kuhakikisha mashabiki wengi wanashudia mechi hiyo TFF imetangaza viingilio mapema VIP A, Sh 30,000, VIP B, Sh20, 000, viti vya Machungwa na Kijani 7,000.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia kwa Ofisa Habari wao, Clifford Ndimbo amesema, tiketi zitaanzwa kuuzwa mapema kuanzia Septemba 20.

“Mchezo wa Simba na Yanga upo kama kawaida na utachezwa siku iliyopangwa, mashabiki wajitokeze kwa wingi kwennda kushabikia timu zao,” alisema Ndimbo.

Ndimbo aliongeza, katika mchezo huo wamezidisha ulinzi wa kutosha ili mashabiki waweze kuwa na amani muda wote wakiwa wanafuatilia mchezo huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!