Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kutekwa Mo: Dereva teksi asomewa mashtaka matatu
Habari MchanganyikoTangulizi

Kutekwa Mo: Dereva teksi asomewa mashtaka matatu

Spread the love

MOUSA Twaleb ambaye ni dereva teksi, leo tarehe 28 Mei 2019, amepandisha katika Mahakama ya Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam akituhumiwa kwa makosa matatu likiwemo la kumteka Mohammed Dewj (Mo). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Shtaka la kwanza, mtuhumiwa anadaiwa kuhusika kwenye mtandoa wa kihalifu ambapo anadaiwa kati ya tarehe 1 Mei na 10 Oktoba 2018 maeno ya Mbezi Beach, Dar es Salaam na Johnsburg Afrika Kusini alitoa msaada kwa wenzake ambapo hawapo mahakamani kutenda vitendo vya jinai kwa nia ya kujipatia fedha.

Shtaka la pili ni kutekanyara, inadaiwa tarehe 11 Oktoba 2018, kwenye Hotel ya Collusium Hotel Masaki, Kinondoni mtuhumiwa na wengine ambao hawapo mahakamani walimteke nyara Mo na kumhifadhi kwa siri.

Shtaka la mwisho ni utakatishaji fedha, inadaiwa kuwa mtuhumiwa akiwa eneo la Mbezi Beach, Dar es Salaam tarehe 10 Julai alijipatia Sh.8 Milioni kwa kujua kuwa pesa hizo ni mazalia ya uhalifu alizozipata kutoka kwenye genge la kihalifu.

Hata hivyo, Wakili Kadushi aliieleza mahakama kuwa, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika sehemu kubwa na kwa kuwa, kesi hiyo ni uhujumu uchumi kuna taratibu zake.

Twaleb (46) amefikishwa mahakamani hapo leo saa mbili asubuhi na kusomewa mashitaka yake mbele ya Huruma Shaidi, Hakimu Mkazi Mkuu.

Mo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Timu ya Soka ya Simba (SCC), alitekwa tarehe 11 Oktoba 2018 alfajir wakati akitoka kufanya mazoezi katika Hoteli ya Colosseum iliyopo Masaki, jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, alipatikana tarehe 20 Oktoba 2019 akiwa ametelekezwa kwenye Viwanja vya Gymkhana ambapo watu 12 walikamatwa wakihusishwa na tukio la kutekwa kwake.

Ukimya wa Jeshi la Polisi baada ya kupatikana kwa Mo ulimkera Rais John Magufuli ambapo tarehe 4 Machi 2019 alisema, ukimwa huo uliacha maswali mengi kwa wananchi.

Rais Magufuli alitoa kauli hiyo wakati akiwaapisha mawaziri Prof. Palamagamba Kabudi na Balozi Augustino Mahige Ikulu jijini Dar es Salaam.

“Mtu aliyetekwa, alikutwa Gymkhana lakini watu wanajiuliza mmmh aliendaje pale, lakini alipowekwa pale na bundeki zikaachwa pale, unajiuliza huyu mtekaji aliamua kuziachaje? Angekutana na polisi wanaomtafuta njiani?” alihoji Rais Magufuli.

Baada ya Mo kutekwa, familia yake iliahidi kutoa donge la Sh. 1 Bil kwa yeyote angefanikisha kupatikana kwake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!